Kigamboni

Steven was born and raised in Dar es Salaam, and moved to Germany for his studies. He graduated with a BSc. in Physics (Jacobs University Bremen), and then a MSc. in Engineering Physics (Technische Universität München). Steven is currently pursuing a PhD in Physics (growth of coatings/multilayers for next generation lithography reflective optics) in the Netherlands. He’s thinking about starting his own business in a few years; something high-tech related. At Vijana FM, Steven discusses issues critical to youths in Tanzania, music, sport and a host of other angles. He’s also helping Vijana FM with a Swahili translation project.

This post has 20 Comments

20
  1. May the Lord Almighty give me time and years to see this plan accomplished. Its such an ideal well and strategically planned. I don’t want to sound cynic, but I can’t help it, as a Tanzanian I know my people. This plan will require sacrifice, hard work and enormous amount of resources.

    But is achievable if we will put our mind to it, we got people, minerals, gas and oil to support the scheme, if the Arabs can do it why not us, they are humans like us.
    What do you think people??

  2. It’s doable, me thinks. Lakini tokea nione hii clip naangalia mambo kwa machale machale hivi… zisije zikawa kampeni tu za “Sisi Emu.” On the other hand, that side of Dar has been too isolated for quite a while — siongelei huu upande karibia na Kivukoni; ukienda ndani zaidi (unaweza ukazunguka na kutokea Mtoni) nadhani pameanza kujengeka siku hizi.

    I would like to hear what other people have to say.

  3. I think they are serious. Kuna project moja ya Bahari Beach..kwa kweli ni kali sana…

    http://www.ipiltd.com/bahari/

    Mi naona haina uhusiano na “si si emu”..manake hawa ni investors wa real estate. Ni more or less the same project as the one in Kigamboni.

    Pia kuna watu ( dutch company) naskia wamenunua lile eneo la salendar bridge, wanataka wafanya land reclamation na wajenge nyumba za makazi…so in 5yrs bongo inaweza ikabadilika sana..

  4. Aisee, lets hope these projects take momentum and become a reality. Our neighbors would die of envy!

    Unajua Kigamboni imekaa vyema kwa mambo kama haya, mtu asikwambie wazee, nchi yetu bomba mno, ila hatuko serious na maendeleo wakuu.

    Kama mipango yote iliopangwa na iko kwenye ma file inapata mavumbi, kama tungeyafanya hayo, aise tungekua mbali mno!

  5. Aliyoainisha Chambi ni ya muhimu hasa. Huko Kigamboni kuna wakazi ambao sidhani huu mpango wanaufahamu unakuja, au kama wanaufahamu sidhani kama wanajua ‘scale’ yake. Tusije baadaye tukafanya kama Mugabe na ‘Operation Murambatsvina’.

    Ila, cha ajabu mpaka leo hii viwanja vinanunuliwa Kigamboni kiholela holela. I just hope when they give you a plot they have the general plan of the future city in mind. Sio kuja kuwekeana “X” baadaye.

    Kwenye video wameonyesha daraja zuri pale Kivukoni dizaini ya Golden Gate bridge (San Francisco). Ili kupata urefu wa kuwezesha meli kubwa za mizigo zipite chini, si itabidi daraja lianzie kilomita kadhaa kabla ya Kivukoni (labda barabara lianzie Sea View). Sijui mainjinia mnasemaje. What about a tunnel?

    Kwenye post iliyopita tumesoma maelezo ya mchoraji Sarah akielezea ubomoaji wa majengo ya kihistoria Dar ili kujenga maghorofa. Kwanini hayo magorofa yasipangwe kujengwa Kigamboni? Identity ya Dar inakufa kabisa. Yaani Dar es Salaam city centre haitakuwa na vivutio vya kihistoria kabisa! No identity!

  6. Kama msemavyo wadau, ni kweli jiji litapoteza historia yake, lakini tukumbuke dunia imebadilika, kuna mijengo ya kizamani zamani pale mjini Dar imekua imezeeka mpaka inahatarisha usalama wa raia, hiyo lazima iondolewe.
    Ile iliokua bado poa itabaki, ila wazee watu hasa wageni wa kizungu wasiseme kuwa hata kwao hawajavunja mijengo ya kizamani, tumekaa kwao, tumeona walivyovunja mijengo yote ya kihistoria na kukaribisha mipya.
    Tatizo la mijengo yetu mipya inakua na upungufu wa mambo fulani, kama parking za chini (underground parking) kwa ajili ya watu wanaotumia hayo maghorofa.
    Lazima tuende na wakati, mijengo mipya inakaribishwa kabisa ili kwenda na wakati.
    Wakazi wa Kigamboni sio tatizo kuwaondoa, tatizo linakuja wakati hao wananchi hawalipwi fidia wanazostathili, hapo ndipo kwenye matatizo.
    Otherwise mie naona plan iliotolewa iko poa, na itatunyanyua kiuchumi.

  7. Mimi nitaelewa wabomoe majengo ya kihistoria labda ili kuongeza upana wa barabara, ila sio ili kubomoa na kujenga ghorofa. Nyumba tunazodhani zinatishia usalama zifanyiwe matengenezo.

    Plan ipo tayari, tujenge maghorofa Kigamboni. Huko ndio biashara nzima ya jiji ihamie – wall street yetu ipatikane huko.
    Maghorofa yafanane na yale ya Hong Kong, au Chicago au Shanghai. Hapo itakuwa mwake, ili watalii wakija wawe na sehemu ya kuiona Dar es Salaam mpya na ile ya kihistoria. Otherwise Dar es Salaam identity yake itakufa.

    Tazama Amsterdam, majengo karibia yote ni ya zamani:
    http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/a/af/Amsterdam_airphoto.jpg

  8. Nionavyo, unaongelea majengo gani ya kizamani waliyovunja huko Majuu? Je, ni majengo ya Kihistoria? Unadhani wanaweza kuvunja Buckingham Palace, Windsow n.k? Pale Posta ya Zamani kuna majengo mengi yenye historia na ni hatari sana kuyavunja badala ya kuyakarabati.

    Hivi lazima tubanane Dar es Salaam tu? Mbona kuna maeneo kibao ya kujenga miji – Kibaha inaweza kuwa New Jersey ya Dar es Salaam. Hapo Chalinze panastahili kuwa mji mkubwa tu, hata pale Segera; kwa ujumla Pwani, Lindi, Mtwara na Tanga inapaswa kuwa miji mikubwa ya kibandari!

  9. Ni kweli chambo usemavyo, lakini ebu tuangalie kama lile jengo la salamander, ebu nieleze sie wabongo tutakosa nini kwa kutokuwepo like jengo pale?
    Au Kuwepo kwa majengo mapya, mie naona faida ni kwetu, kwanza watu wengi zaidi watapata ofisi za kupanga na yako salama zaidi.
    Kuvunjwa kwa majengo yale yenye maana sana kama kanisa la Azania front haitawezekana, sasa ukiangalia wizara mbili tatu, zilikua kwenye majengo ya kihistoria sawa, lakini hayakuwa salama na hayakutosheleza kidhi za wizara, hayo sidhani kama mnalamika kwa kuyakosa wazee?
    Ila nawaelewa na naomba mkumbuke, kama mijengo imejengwa zamani na haina kasoro, sidhani kama wahusika watathubutu kuyavunja.

  10. Nionavyo, nadhani swali muhimu hapa ni je, maendeleo yanapimwa kwa nini – ‘vikwangua anga’? Kama suala ni kipato hebu angalia jiji la London linaingiza shilingi ngapi kwa siku kutokana na utalii katika majengo yake ya zamani. Hii Dar es Salaam imeshajaa pale katikati ya mji, kilicho muhimu sasa ni kuondokana na uhodhi wake kama jiji kuu hapa Tanzania. Hizi foleni zinasabababishwa na ukweli kuwa huu mji haukupangwa kukua kupita kiasi ilhali hakuna sehemu zingine za kuchuja ongezeko lake la mzunguko wa watu na fedha jijini. Sasa tunapaswa kujenga miji mingine mikubwa ili kupunguza watu Dar es Salaam. Kwa kuanzia miji yote inayopakana na bahari ya Hindi inapaswa kujengwa ili iwe mikubwa kama Dar es Salaam. Ile bandari ya Bagamoyo ijengwe kabla JK hajamaliza muda wake halikadhalika ile barabara ya kutoka Dar es Salaam kwenda Tanga kwa kupitia Msata, hii itasaidia sana kufupisha safari za kwenda Kilimanjaro na Arusha na pia kuipunguzia mzigo barabara ya Morogoro – halikadhalika itasaidia kukua kwa mji wa Tanga na Bagamoyo (bila kuathiri majengo yake ya zamani natumaini)!

  11. Chambi.

    Sasa ndio linakuja lile swala linalozungumzwa sana jijini, la “satelite town”.
    Mipango na ramani zote iko tayari, swala ni wahusika kujipanga na kuruhusu hela za kuanza kazi. Lini hili litaanza ndio kasheshe yetu watanzania.
    Hizo barabara uzisemazo nazo washapanga, tena tunasubiri lini watatenga hela na kazi kuanza.
    JK alishaahidi nafikiri, kwamba kabla hajaondoka, basi kutakua na port mbegani na ka airport kadogo kama kale ka kwetu kazamani.
    Chambi mipango wanayo, tatizo kwa ni kutenga hela na utekelezaji tu, ofcourse na jinsi watakavyotekeleza!

  12. United African University of Tanzania. I just hope this won’t be the name of the University there or anywhere for that matter. They can do better than that 😀

  13. hey.. mi jamani nimefurahi kuona kumbe kuna watanzania wenzangu kama mimi ambao tunaitakia maendeleo nchi yetu.. nimesoma maoni yenu na yote ni ya muhimu… kila mtu anajaribu toa mawazo kwa jinsi anavyoona yeye… na hizi ndo changamoto zenyewe…. ila kwa hii project.. mi nina amini itawezekana na itamalizika kwa muda uliopangwa…. ila tusisubiri eti mpaka tuone umekamilika… tuwe part of it.. tuchangie katika kuwahamasisha watanzania wengine tuweze kuweka katika vitendo…. hii project inamuhusu kila mtanzania.. hata kama pesa zitatolewa ila bila juhudi zetu sisi wenyewe hatutoweza…. Wengi wetu watanzania hatuna vision ndo maana tukiona vitu kama hivyi tunaona kama danganya toto…. hapa hakuna swala la u ccm wala u chadema, u cuf… kama ni maslahi ya taifa embu wote tuinuke na ku support taifa letu kwani nchi zingine zimeweza kwanini sisi tushindwe?????

  14. Mimi nina hofu na idadi ya wakazi waliotajwa, kigamboni kuna watu wengi sana,ukitaka kujua angalia vivuko vinavyofanya kazi muda wote na huwa vinajaa watu, watu wengi wanaweza kuachwa bila makazi

  15. MIE HUWA SIAMINI KWANZA HATA HII VIDEO NI YA UONGO COZ KUNA STESHENI MOJA YA ULAYA WANAZO HIZI INAITWA WORLD DISCOVERY WANAONESHA JISHI MAJENGO, MADARAJA, NA BARABARA CHINI YA MAJI NA MIAMBA WALIVYOJENGA, WAME-EDIT KWA KUJUA KUWA WATANZANIA WENGI HAWAWEZI KWENDA NET

  16. HIVI ULISHAONA WAPI VIDEO YA PLANING YA MJI INAONESHWA BILA ENGENEER KUONESHA KUWA HILO DALAJA LITAKUWA LA VIPI, WAACHE KUTUZINGUA BAADHI VIPANDE VINGI VYA PICHA VIKO KWENYE WORLD DISCOVRY WAMEUNGAUNGA VIPANDE NA KU-EDIT IMAGES, HAAAA! HAAA!!!! MTAWAPATA HAO

  17. Nawaomba watu wa Antiquity na watu wa cultural heritage managment waweliangaliae suala la majumba ya zamani Tanzani hasa kwa miji ya pwani mwa East Africa ihli tubaki na kukumbu ya kutosha na si hali inayoonekan asaasa ya kubomoa majengo ya zamani na kuinua mengine ambayo hata hayendani na miundo mbinu ambayo aiongezeki kulingana na ongezeko la majengo yenyewe.
    Watu wa mipango miji najua wamekuwa wakitoa mawazo yao lakini hayatenewi kazi kwasasbabu za kisiasa na iteerest za watu fulani fulani hapa nchini kwani inaonekan hat amiji inayo kuwa bado utekelezaji wa mipango miji bado haufuatwi sawasawa.

  18. SAID,

    Iko wapi hiyo video waliyokopi? Naomba link kama iko online.

    Ila upande wa pili kukopi sio tatizo. Majengo mengi tu ni kopi za mengine. Na tayari kuna project iliyokamilika kama vile hostels za UDOM, ambayo ni kopi ya Mabibo Hostel.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend