Elimu ya sekondari Tanzania: Maafa

Is the Tanzanian government investing in the right ingredients? Courtesy: www.moe.go.tz

A whopping 50% — some 174,193 of 17-18 year olds — failed last years Form Four examinations. Where are we headed?

Related links:

Previous ArticleNext Article
Joji was born and grew up in Dar es Salaam, Tanzania. He graduated with a B.Sc in Biochemistry in Germany, and is now pursuing a Masters degree in Microbiology & Immunology at the Swiss Federal Institute of Technology (ETH) in Zurich, Switzerland . Joji is particularly interested in matters related to global health, and basic science research that tackles public health challenges. He is engaged in mentoring Tanzanian students in higher education issues, most notably at the Kibaha High School. In this capacity, Joji blogs with Vijana FM about scientific research and development, and how youth can gain greater access to higher learning.

This post has 24 Comments

24
  1. Tunahitaji a re-examination of the curriculum being taught, as well as an impact assessment of investments flowing into the education sector.

    On top of all that, I personally think we need to redefine what education means today.

  2. tumeongeza shule nyingi sana za kata katika kipindi hiki cha miaka mitano, lakini shule hizi zinakosa walimu , nyingine hazina vifaa vya kutosha, nafikiri hizi zinachangia 50% ya wanafunzi waliofeli, je kulifanyika utafiti wa kutosha kabla ya kutekeleza shule za kata? Je kwa nini tulifocus zaidi kwenye wingi wa shule , ambapo kuna nyingine ni majengo tu maana hata wanafunzi hakuna, tusingeweza kutumia fedha hizo kujenga shule chache kutokana na uhitaji wa maeneo husika na kisha fedha nyingine zikatumika kuboresha vifaa, na pia tungesevu walimu ambapo hizi shule chache ambazo zingekuwepo kulingana na mahitaji zingekusanya walimu wa shule ambazo ni majengo tu na wanafunzi ni wachache au hakuna, nafikiri tulijali zaidi kutengeneza statistical data zaidi ya ubora wa elimu.

  3. Tumeshalaumu na kutukana sana. Wakati tunaendelea kujadili haya, kama mambo yakiendelea kama yalivyokuwa kwenye hii miaka minne iliyopita, basi tutajikuta tuna pengo kubwa la wananchi/vijana wasio na ujuzi (elimu ya kutosha) kwenye nyanja mbalimbali.

    Hili pengo linaweza kuwa kati ya miaka 5 – 15, kutegemea na mtazamo wako. Tunajua kuwa baadhi ya hawa ambao hawakufanya vizuri, wataishia kwenye vyuo vya ualimu (kama mnavyojua, ndio desturi yetu).

    Kuna mtu anajua kuhusu vitu vyovyote vinavyojadiliwa wizarani sasa hivi? Au ndio ule mpango unaingia kwenye ngwe ya pili tu? Zile ripoti za Uwezo na asasi nyingine, zinachukuliwaje?

    Kama watu wanafanya kazi zao (trying to be optimistic), matunda ya mabadiliko yatachukua muda mrefu. Hiki kizazi ambacho ndio kinanyimwa haki yao ya kupata elimu ili kujikwamua kimaisha, kitafanya nini? Miaka 10 — kwa mwendo huu — itazaa wengi…

    Ningependa kusikia hoja za watu; nini kifanyike? Tuanze upya; halafu, tuanzie wapi na tufanye nini? Serikali na wananchi kwa ujumla.

  4. M Masesa
    Mtaa wa Bububu
    Mwisho wa upepo
    Daresram

    Jakaya M Kikwete.
    Ikuru,
    Daresram.

    Ndugu Raic.

    YAH: Matokeo yangu ya kidato cha nne

    Boc natumaini ulifika salama Swaziland kwenye mkutano wa Davos. Naona Tanzania ndio 2mekuwa kiranja wa nchi mackini duniani kila mwaka iwe sisi tu ndio 2we wawakilishi wa mackini wote, isingekuwa noma ukiuchuna baadhi ya miaka, 2waachie angalau na nchi kama Chad au Somalia wapate nafac.

    Wakati ukipunga upepo huko na kushiriki makongamano yasiyoisha miaka nenda rudi, ningeomba upate nafac kufuatilia matokeo yetu ya kidato cha nne. Cio ciri hizi skonga za kata ulizozileta kusema ukweli ulifanya blanda. Nimeshikwa na bumbuwazi kwani bado ciamini kweli nimepata mswaki katika masomo yote, ukizingatia kwamba nilikuwa shabiki wako nambari wani ktika kampeni, na hata uliposema azalani kuwa hata wewe hesabu hazipandi nirifarijika mno. Ira ckuzani nitafeli.

    Ninashauriana na wenzangu turioferi hapa ktk kata yetu ili tuanze mchakato kufungua mashitaka maakamani kuishitaki wizara ya elimu kwani haki ye2 ya kupata erim bora imebakwa laivu bila chenga, kutokana na kuturubuni kwe elimu ya sekondari za kata, bila ya kuwa na walimu, vifaa, au dira ya ni nini miaka 4 ya sekondari inabidi inisaidie kuelimika.

    Je ni haki mimi kama mtanzania ndoto zangu zikatwe kwasababu nimepata Div 0, kisa nilihukumiwa kusoma ktk shule ya kata?

    Haingii akirini kwa mtu mwenye akiri timamu akae na kuamini mipango yote unayoifanya au unayotaka kufanya kama yanamanufaa yeyote. Uliongea kwa cana tu kuwa umeleta mapinduzi kielimu, leo hii hoja zako zimegonga pua na maisha ya vijana laki 3 kama mimi umeyaalibu. Nackia unaongelea mpango wa kujenga barabara serengeti, je una uhakika baada ya miaka 5 hatutakuja kukushtaki pindi soko letu la utalii likifa?

    Pries, fanya maamuzi yenye busara na cio kila kitu kiwe kiciaca. au vipi. Im very disaponted very raight now. Nimeandika kwa kingreza ili kuonyesha mcictizo.

    ndimi.
    mwanafunzi Shule ya Sekondari ya Yusuf Makamba, Daresram

  5. Mimi ninacho ona hapa ata hao walikofaulu walichopata ni kweli wamepewa kwa kwa msingi madhubuti au walio na uwezo wa kukariri wa wachahce ndio hao tumeona wamefaulu hebu angalia huyo mwananfuzi hapa juu aliyeandika comments hata kuandika dar es salaam vizuri kuna mshinda mimi wasi wasi wangu ni ata hao waliopata division one sijui kama wamepata elimu nzuri au ni elimu ya kujibu mitihani vizuri mfumo wetu wa elimu tuubadilishe hautufai utukuta mwenye division four ndio anaweza aka reason vitu vizuri zaidi ata huyo aliyepata division one

  6. Tuseme mara ngapi … ujenzi si elimu. Bila walimu, tena bila walimu waliofunzwa vema, bila vitabu, bila madawati, yale majengo ni ghala si shule!
    Aidha sera ya Kiingereza kama lugha ya kufundishia hadi lini. Angalau 30% ya kufeli huko ni kwamba hawana Kiingereza cha kutosheleza darasa la pili, si Kidato cha pili. Lugha inatumika kama njia ya kuwafelisha walio wengi, wakiwemo wanasayansi kibao ambao wanajulikana mara nyingi si wataalam sana wa lugha

  7. Hii ni hatari inayotokea tunapoamua kuongozwa na fikra za wanasiasa na kubeza maoni ya kitaalam.

    Shule za kata ni mtaji wa kisiasa, lakini si kitaalamu.
    Zinasaidia kuboresha takwimu za idadi ya shule, vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo nk. [Mtaji safi kwa kura za wasiofikiria].
    Lakini katu hatusaidii kuboresha elimu kwa namna hii. Na bila kuwekeza kwa dhati katika ubora, tunapalilia ufa mkubwa uliopo kati ya wenye nacho[wanaosoma na wanaowasomesha watoto wao shule bora za gharama kubwa] na wasio kuwa nacho [wanaosoma na kusomesha shule za kata].

  8. Mdau, tovuti ya wahusika ipo pale juu; itakuwa sio vibaya ukawauliza wahusika AU ukakokotoa mwenyewe.

    Kwa upande mwingine ni swali zuri — hivi mishahara ya walimu imeongezeka kwa kiasi gani? Mishahara yao nao ilikuwa adjusted accordingly (re: inflation)?

  9. Inasemekana mwaka juzi (2009) performance ya f4 ilishuka sana, mwaka jana (2010 – matokeo haya ya sasa) performance imezidi kushuka…

    Nilivyodadisi matokea ya 2009, nikaambiwa ndio f4 results za kwanza tokea kuanzishwa kwa shule za kata (nimesikia wengine wanaziita shule za Lowassa)

    Naomba tusaidiane katika kufanya huu utafiti….

    Hoja: kabla ya kuanzishwa shule za kata wanafunzi wa ngapi walikuwa wanaingia f1?? na baada ya kuanzishwa shule za kata ni ongezeko kiasi gani la wanafunzi wanaoingia f1??

    Fikra: Yawezekana kabla za kuanzishwa shule za kata mchujo ulikuwa unafanyika Darasa la Saba (waliokosa kujiunga na f1 tunaambiwa hawajachaguliwa sio kwamba wamefeli)….. baada ya kuanzishwa shule za kata mchujo sasa hivi unafanyika kwenye mtihani wa taifa wa f4.

    Hii ni fikra tu, tusaidiane kutafuta data halafu tuzidi kujadili…

    Huu utafiti mdogo waweza kusaidia kugundua tatizo lipo wapi na kujenga hoja yakurekebisha!!!!

  10. @Mdau. Umeraise point muhimu kuhusu adjusted figures, i.e., inflation. Ila hapo tutakuwa tunakimbia mada halisi. The said graphs were chosen ili mwenyewe upate a qualitative impression on the education expenditure vis-a-vis student performance, hivyo tuweze kujadili ni yepi tufanye so that we can create a turn-around in student performance.

    In fact ukitaka kupata an accurate representation of students who passed one should look at the actual numbers of students passed and not percentages, kwani ingawa percentage ya waliofaulu katika mwaka fulani ni ndogo, yawezekana idadi halisi ya waliofaulu ni wengi zaidi kuliko mwaka uliopita, mf: kutokana na ongezeko kubwa la waliojiandikisha kufanya mtihani ukilinganisha na miaka ya nyuma. (in this case you will eventually realise that many – in terms of absolute numbers – have failed as well. So back to square one)

    Kurudi kwenye mada, tufanye nini ili kuondoa ulipuaji kama huu katika sera za maendeleo? Do our policy makers see problems as multifaceted?

    Elimu bora > jenga shule kila kata (mambo ya waalimu, vifaa, mitaala baadaye)
    Afya bora > jenga hospitali kila eneo (mishahara ya wauguzi, unafuu wa dawa, usafi wa jiji tutayawaza baadaye)

    PS: Waliomaliza kidato cha nne 2010 ndio Form Four wa kwanza katika shule za kata. JK aliingia madarakani mwishoni mwa 2005, 2006 shule zikaanza kujengwa. 2007 wanafunzi wa kwanza kuanza Form 1. 2010 ndio tumepata gradutes wa kwanza ambao zaidi ya 80% ya wanafunzi wa shule hizi wamefeli.

  11. Simple; retain the brightest minds and heads as teachers but this will not be cost free. Its time to pay good salaries to these minds.

    Mfano: Ukiweka standard kuwa mwalimu yeyote wa sekondari aliyepata madaraja ya kwanza katika form four and six mshahara kwa mwezi ni take home ya Tshs 2m. Kama atapata daraja la kwanza chuo cha ualimu mshahara ni take home Tshs 4m. Kama huyuhuyu atapata at least daraja la pili la juu(upper second) chuo kikuu mshahara ni take home ya Tshs 6m. Tutakuwa na walimu watakaokuwa tayari kutumia nguvu na akili zao zote kwa ajili ya kutoa elimu bora.

    Unapowapa nafasi ya kufundisha walimu wa UPE halafu kutunga mitihani unawatumia brightest minds ni lazima kusiwe na compatibility kama matokeo yanavyoonesha.

    Nchi za wenzetu walimu wanalipwa kutokana na standard zao kwetu sisi ni generalisability yaani division four na one unawaweka chungu kimoja linapokuja suala la ualimu. South Korea wanaitwa walimu ni Nation builders na wanapewa nafasi kubwa sana katika jamii. Sisi mishahara mikubwa na malupulupu yote tunalimbikiza kwa wanasiasa, wabunge tunasahau “front liners” na matokeo yake ni haya. Serikali inaposema haina pesa za kuwalipa walimu mshahara huo wakati wabunge wanalipwa mshahara wa mwezi mmoja unaowalipa walimu kumi ni kutokuwa na kipaumbele na ubinafsi wa wanasiasa.

  12. I actually think uki-consider annual decrease of the value of hela ya madafu yetu, kuna uwezekano mkubwa hizo billioni hapo juu zina thamani ile ile, ni miaka tuu imebadilika. regardless, bado matokeo hayakubaliki, and siamini ni madogo wajinga, it is about time the govt reviews the current curriculum, ffs, madogo wanasoma vitu tulivyosoma sisi — madogo wanatakiwa wasome vitu vitakavyowaanda na mbio za karne hii sio za enzi ya Mwinyi, I bet ndiyo maana na wenyewe wakizama class wanaona kichina tuu… kitabu kinatumia mifano ya 1960s to clarify points za 1960s, kweli utaelewana na madogo! States almost kila semester wanafunzi wanatumia kitabu kipya.

    PS. naomba hii ngoma ichukuliwe kama constructive criticism sio hating…lol… jus sayin

  13. kwa kweli hii ni balaa yaani ni aibu kweli kwa nchi yetu hii ya Tanzania,je kwa hali hii kuna mtu atajaribu kuajiri engineer kutoka humu Tanzania kweli?je tutaweza kujitegemea kama Tanzania kweli? maana tunapoelekea ni kumaliza nguvu kazi ya taifa na kuzidisha umaskini.serkali mko wapi jamani? naombeni muangalie ili tatizo kwa kweli na nyie wanafunzi.whenever you get an opportunity use it effectively unajua wanafunzi msilalamike maana kunawengine waliitafuta hata hiyo nafasi ya kusoma shule za kata walikosa lakini nyie mmeipata mnalalamika.jamani wanafunzi wenzangu tubadilike tuanze kujitegemea sisi kwa sisi maana kwa kweli hii ni unfair kwamba wengine wanaifaidi nchi while wengine wanateseka hii ni unfair lakini tutafanayaje wananchi kosa tulilfanya sisi tulidhani kuweka mfumo mmoja wa utawala kutapunguza matatizo lakini kumbe tunaongeza matatizo jamani miaka mingine ijayo msifanye makosaaaaaaaaaaaaaaa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

  14. TUACHE SUALA LA SIASA KATIKA ELIMU. TATIZO LA KUSHUKA KWA KIWANGO CHA ELIMU HAPA NCHINI HASA MATOKEO YA KIDATO CHA NNE NI MOJA TU. WALIMU WANA MGOMO BARIDI, HII NI BAADA YA SERIKALI KUWANYIMA FURSA YAO YA KUANDAMANA, PIA KUGOMA ILI KUSHINIKIZA KULIPWA MAFAO YAO.

    HEBU JIULIZE ITAKUWAJE MWALIMU AFUNDISHE TUITION CHINI YA MNAZI NA ATOE WATOTO WENYE DIVISION I, II NA III, WAKATI HUO MWALIMU HUYO SHULENI ANAKOFUNDISHA HAKUNA HATA ALIYE PATA DIVISION III?

    WALIMU WA TANZANIA WAMEKATA TAMAA NA MAISHA MAGUMU HIVYO KUWAFANYA KUONGEZA NGUVU KATIKA TUITION AMBAYO INALIPA KULIKO SERIKALI. HIVI VIONGOZI HAWANA HATA AIBU WAO WANALIPWA ZAIDI YA SH MILIONI KUMI NA MBILI (12,000,000/=) ILI HALI ALIYEWAPA UJUZI ANALIPWA CHINI YA LAKI MOJA NA NUSU (150,000/=). NDUGU HATA KAMA WEWE NI MJINGA HUWEZI KUKUBALIANA NA HALI HII YA KIUNYONYAJI KUPITIA MSEMO WA AMANI NA UTULIVU.

    ONYO KWA SERIKALI BAADA YA WANANCHI KUPIGWA MABOMU BARIDI NA PENGINE YA MOTO SASA WAMEAMUA KUWA NA MIGOMO BARIDI NA MATOKEO YAKE NI KULIPUKA MABOMU (MBAGALA NA GONGO LA MBOTO), KUONDOLEWA KWA MATAALUMA YA RELI NA PENGINE KUANGUKA KWA RELI, MATOKEO MABAYA YA MITIHANI. IKUMBUKWE YALE YALIYOTOKEA MISRI HATA TANZANIA YAWEZEKANA HASA KAMA HALI YA VIONGOZI HAITABADILIKA. MUNGU IBARIKI AFRIKA. MUNGU IBARIKI TANZANIA.

  15. tanzania tusifikirie jinsi ya kutoa mitihani ya kidato cha pili kabisa kwani matokeo yake ni kama haya ya wanafunzi wengi k,ufeli na selikali husika kufumbia macho.
    TUTAZAME SHULE ZA VIJIJINI ZILIVYO.
    FROM MUCCOBS

  16. Labda mambo ya kujiuliza ni kwa namna gani elimu yetu ya sekondari kwa sasa inaweza kutufanye tuwe “competitive” ndani na nje ya Tanzania…kuna kitu chochote cha kujivunia!?

    Elimu yetu inatubadilisha kwa namna yeyote chanya au ndo tumeendelea kusoma ili tujibu na kufaulu mithani.Tusipoangalia elimu yetu tena na mifumo kwa ujumla kama alivyosema AK hapo juu tutakuwa tunatwanga maji kwenye kinu tu.

    Pengine imefika wakati mfumo inabidi ubadilike…lakini pia content inayofundishwa na mfumo mzima kwa kutoa mitahani inabidi ubadilike kuendana na nyakati tulizopo.

  17. Kushuka kwa maadili kwa watoto wetu kunawafanya kuchukulia suala la kusoma kama mzaa tu, jamani hebu fikiria watu wa zamani waliosoma enzi za mkoloni chini ya nidhamu kali walivyoweza kufaulu vema katika masomo yao ila leo hii tunazuia viboko na adhabi nyinginezo mashuleni hivi kweli mwanafunzi ataweza kusoma kwa umakini? hebu tubadilike watanzania

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Send this to a friend